CHAMA kipya cha siasa nchini kijulikanacho
kama Tanzanian Patriotic Front, kimezinduliwa jijini Dar na Msajili wa
Vyama vya Siasa, Jaji Fransis Mutungi kutoka kwa waanzilishi wa chama
hicho, Deonatus F. Mutani na Optatus B. Likwelile.
Chama hicho kimezinduliwa leo kwenye Ofisi
za Msajili wa Vyama vya Siasa jijini Dar mbele ya waandishi wa habari
ambao walishuhudia waanzilishi wa chama hicho wakipewa cheti cha
usajili.
Katika uzinduzi huo, Jaji Mutungi amesema
kwa mujibu wa sheria na taratibu za usajili wa vyama, waanzilishi wa
chama hicho watakiwa kuhakikisha wanafuata vigezo vinavyohitajika
ikiwemo kuzunguka mikoa 10 ya Tanzania Bara na Serikali ya Zanzibar
kupata wanachama wasiopungua 2000 ili kuweza kupata usajili wa kudumu.
(NA DENIS MTIMA/GPL)

Note: Only a member of this blog may post a comment.