BRIGHTON MASALU
CHIZIKA! Wakati hekeheka za maandalizi
zikipamba juu ya ndoa ya karne ya staa wa sinema za Kibongo, Wolper,
mwanadada huyo anaonekana kuingiwa na ‘uchizi’ juu ya suala hilo ambapo
muda wote anawaza ni kwa namna gani ataweza kuweka historia juu ya
shughuli yake. Akizungumza na Ijumaa Wikienda, hivi karibuni ndani ya
Ukumbi wa Jozi.
Village, jijini Dar, Wolper alisema:
“akili haijakaa sawa kabisa, nawaza juu ya ndoa yangu ambayo muda si
mrefu itatimia, silali, sili na sipumui vizuri, kila kitu kimesimama, ni
kama imenitia uchizi, muda wa kuishi na mwanaume kwenye ndoa takatifu
umewadia,” alitiririka Wolper.
Note: Only a member of this blog may post a comment.