Wanasayansi wametengeneza dawa kutumia ndizi zinazoweza kuua virusi vya aina mbalimbali vikiwemo vya HIV, Hepatitis na mafua.
Inatumainiwa kuwa dawa hivyo mpya inaweza kuwa na muhimu katika
kupambana na virusi vingi hatari. Dawa hiyo iligundulika miaka mitano
iliyopita na kuaminika kuwa tiba ya virusi vya HIV lakini ilisababisha
madhara ambayo wanasayansi sasa wamekabiliana nayo.
Dawa hiyo iliyopewa jina la BanLec inayoweza kupambana na virusi
kwenye panya lakini haileti madhara. Watafiti wanaamini kuwa dawa hiyo
inaweza pia kuponya Ebola.
Hata hivyo walionya kuwa ulaji wa ndizi wa kawaida hauwezi kuwa na matokeo yale yale.

Note: Only a member of this blog may post a comment.