Imelda Mtema
WATANGAZAJI wa Shindano la Bongo Star Search,
Penniel Mungilwa ‘Penny’ na Siza Daniel wamenaswa wakioneshana mahaba
hadharani kama mtu na ‘bebi’ wake.
Tukio
hilo lililopigwa chabo na paparazi wetu lilijiri wikiendi iliyopita
maeneo ya Kawe Beach, Dar wakati wawili hao walipokuwa wakijiandaa
kurekodi kipindi cha shindano hilo ambapo walionekana kushea juisi
ambayo kuna wakati Siza alimnywesha Penny huku wakati mwingine, Penny
akijibu mapigo.
Wawili hao baada ya kupigwa picha na paparazi wetu na kuwauliza kama
ni wapenzi, Siza alishindwa kuzungumza lolote lakini Penny alipoulizwa
kama jamaa huyo ndiye mrithi wa Diamond (Nasibu Abdul), alijibu kwa
kifupi:
“Jamani kusoma hujui hata picha huoni?”

Note: Only a member of this blog may post a comment.