Chande Abdallah
Mchekeshaji maarufu
Bongo, Rashidi Mwinishehe ‘Kingwendu’ ameweka wazi kwamba yupo njiani
kuachana na mambo ya uigizaji mara baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge.
Akizungumza na mwandishi wetu, Kingwendu
ambaye anagombea nafasi ya ubunge katika Jimbo la Kisarawe kwa kupitia
tiketi ya CUF, amesema kwamba kwa sasa kitu anachokifikiria ni
kuwatumikia wananchi kupitia siasa.
“Nimepanga kuachana na uigizaji, sitaki
tena, ninatarajia kesho kuchaguliwa kuwa mbunge, ni mafanikio yangu na
Bongo Muvi pia, hivyo sitaweza kuendelea na uigizaji, ninataka
kuwatumikia wananchi kupitia siasa,” alisema Kingwendu.

Note: Only a member of this blog may post a comment.