Saturday, October 17, 2015

Anonymous

Dakika 7 za CCM Mbeya na UKAWA Mwanza ! Yanayomuudhi KINANA...LOWASSA Waliomsubiria Hotelini (+Audio)

Zimebaki siku tisa tu mpaka kuifikia October 25 2015 siku ya uchaguzi mkuu Tanzania ambao upo kwenye headlines na CCM, UKAWA na ACT WAZALENDO pamoja na vyama vingine vinavyoshiriki. 

Post hii ni maalum kukukutanisha na matukio ya Mwanza na Mbeya ambako CCM na UKAWA wamehusika ambapo kwa Mwanza, ni mgombea Urais wa UKAWA Edward Lowassa alivyokua akisubiriwa nje ya hoteli aliyofikia, watu walikua wakikaa nje kwa saa kadhaa ili kumuona, unaweza kusikiliza ilivyokuwa kupitia hii sauti hapa chini. 

Kwa upande wa CCM Mbeya, Katibu wake mkuu Abdulrahman Kinana aliongea na Wananchi na nina mnukuu akisema ‘Sisemi kwamba CCM hatujafanya makosa, tumefanya makosa na tumekuwa na kasoro pamoja na mapungufu lakini nani asie na mapungufu? tumejitahidi wengine walaji wengine waporaji, wengine hawasaidii Wananchi, wengine uongozi kwa maslahi yao… haya ni mambo tunahangaika kubadilisha kila siku
Ukitaka kumsikiliza zaidi Katibu mkuu Abdulrahman Kinana na Wafuasi wa Edward Lowassa unaweza kubonyeza play hapa chini….

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.