Imelda Mtema
STAA wa sinema za
Kibongo, Kajala Masanja, amefunguka kuwa anamshukuru Mungu uchaguzi
umefika kitu ambacho alikuwa akikiomba usiku na mchana.
Akizungumza na gazeti hili, Kajala
alisema katika kipindi chote cha vuguvugu la uchaguzi kuna vitu vingi
vililala kutokana na kila mmoja macho,masikio,akili na hata mawazo
vilikuwa ni uchaguzi hivyo kushindwa kufanya chochote.
“Namshukuru Mungu huu uchaguzi umefika
maana ilikuwa ni majanga makubwa hakuna kitu ulichokuwa unaweza kufanya
katika kipindi chote cha kampeni jamani ila nachoomba zaidi ni amani,”
alisema Kajala.
Uchaguzi Mkuu wa rais, wabunge na madiwani nchi nzima unatarajiwa kufanyika kesho.

Note: Only a member of this blog may post a comment.