Saturday, October 24, 2015

Anonymous

Afadhali UCHAGUZI Umefika -KAJALA

kajala
Imelda Mtema
STAA wa sinema za Kibongo, Kajala Masanja, amefunguka kuwa anamshukuru Mungu uchaguzi umefika kitu ambacho alikuwa akikiomba usiku na mchana.
Akizungumza na gazeti hili, Kajala alisema katika kipindi chote cha vuguvugu la uchaguzi kuna vitu vingi vililala kutokana na kila mmoja macho,masikio,akili na hata mawazo vilikuwa ni uchaguzi hivyo kushindwa kufanya chochote. 
“Namshukuru Mungu huu uchaguzi umefika maana ilikuwa ni majanga makubwa hakuna kitu ulichokuwa unaweza kufanya katika kipindi chote cha kampeni jamani  ila nachoomba zaidi ni amani,” alisema Kajala.

Uchaguzi Mkuu wa rais, wabunge na madiwani nchi nzima unatarajiwa kufanyika kesho.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.