Friday, September 11, 2015

Anonymous

Wakiwa Bize na Siasa, Mimi Nauza Mkaa Wangu -ESTER KIAMA

ester-kiama
Imelda Mtema
Staa wa muvi Bongo, Ester Kiama ameibuka na kusema kuwa wakati mastaa wenzake wakihangaika na kampeni za siasa yeye anauza mkaa wake kwani amegundua kuwa wamemtenga kwa sababu hawajawahi kumshirikisha kwenye lolote. 

Akizungumza na Ijumaa, Ester alisema kuwa awali alikuwa akiumia kuona ametengwa lakini alipokaa na kufikiria kwa makini aliona ni bora alivyoachwa ili aifanye kazi yake ya kuuza mkaa kwa ufasaha.
“Nilikuwa naumia na kusema nimetengwa lakini wamenisaidia kwa upande mwingine, huu ndiyo wakati wa biashara kwani mvua inakuja mpaka kampeni zinaisha nitakuwa nimeingiza fedha nyingi kuliko waliojikita kwenye siasa,” alisema.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.