MTANGAZAJI
matata wa Bongo Star Search (BSS 2015), Penniel Mungilwa ‘Penny’ wiki
iliyopita alijikuta akiangua kilio bila aibu baada ya majaji wa
shindano hilo kutaja washiriki waliokuwa wakiaga.
Akipiga stori Amani, Penny alifafanua
sababu ya kushindwa kujizuia kuangua kilio ni kutokana na kwamba mara
nyingi anakuwa na washiriki hao na ameshawazoea sasa aliposikia wanaaga
shindano hilo aliumia sana.
“Unajua wale washiriki ni kama rafiki
zangu nimewazoea sana, wanapotajwa na majaji kuwa wanaaga shindano hilo,
nilishindwa kujizuia na kujikuta machozi yakinitoka,” alisema Penny.

Note: Only a member of this blog may post a comment.