Thursday, September 17, 2015

Anonymous

MAGUFULI APOKELEWA KAMA MFALME KIGOMA,WANANCHI WAKIRI ATOSHA KUWA RAIS

Mgombea urais kupitia CCM, Dk John Magufuli jana alipata mapokezi ya kishindo mjini Kigoma alikofanya mkutano mkubwa na wa kihistoria.
Dk Magufuli alipokewa na umati mkubwa wa wananchi waliofurika katika uwanja wa Kawawa kwa ajili ya kumsikiliza.

Akiwahutubia maelfu ya wananchi hao, Dk Magufuli aliwaomba wananchi hao kumchagua kuwa rais kwa kuwa atachagua mawaziri watakaowatumikia wananchi kwa nguvu zao zote na wataongozwa na waziri mkuu makini.

“Nitateua mawaziri ambao wataweza kwenda na kasi ya maendeleo mtakayohitaji, nitasimamia mimi mwenyewe pamoja na waziri mkuu makini na watakuwa tayari hata kuumwa na mbu, kunguni wakati wote ili mradi wawatumikie watanzania hata usiku wa manane,” alisema.
Magufuli pia aliahidi kuwa serikali yake itawajali walemavu, wasanii pamoja na wanamichezo ili kuongeza kasi ya maendeleo yenye tija kwa taifa.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.