Ikiwa ni katika muendelezo na harakati za kuipeleka klabu ya soka ya Simba katika mfumo wa kisasa na kujenga kikosi chenye wachezaji wenye morali uwanjani, mwezi September klabu ya Simba imetangaza kuanzisha mfumo wa kumtafuta mchezaji bora wa mwezi. 
Kupitia kwa Rais wa klabu hiyo Evans Aveva
 ametangaza kuanzisha mpango huo mwezi September, ambapo mfumo 
utakaotumika kumpata mchezaji bora wa mwezi ni mashabiki ndio watakuwa 
na nafasi ya kumchagua kwa kumpigia kura kwa njia ya sms. 
“Wanachama
 na wapenzi wa Simba wanathamini mno mchango wa wachezaji katika 
kuifanya timu yetu ifanye vizuri, hivyo tumeona ni jambo la busara kuwa 
klabu ya kwanza Nchini Tanzania kuwa na tuzo ya mchezaji bora wa mwezi. 
Tunaamini kuwa Tuzo ya mchezaji bora wa mwezi wa Simba itaongeza 
morali na kujituma kwa wachezaji wetu” >>> Evans Aveva
 

 
 
 
 
Note: Only a member of this blog may post a comment.