Bondia Floyd Mayweather amesisitiza kwa mara nyingine kuwa Andre
Berto ndiye bondia wa mwisho kupigana naye katika pambano lao la
Jumamosi.
Mayweather amesema watu wengi wanafikiri tofauti kwamba atapigana
tena. Pambano hilo la 49 ndilo litakuwa la mwisho kwake na anataka
kushinda kubaki na rekodi yake ya kutopigwa daima katika ngumi za
kulipwa.
Pambano hilo litafanyika Jumamosi katika Ukumbi wa MGM Grand Garden
jijini Las Vegas, Marekani na tayari tiketi zimeanza kuuzwa na
zinakaribia kuisha.

Note: Only a member of this blog may post a comment.