Naibu Waziri Mambo ya Ndani,
Pereira SilimaWAKATI kura za maoni zikileta shangwe na vilio kwa makada
wa Chama Cha Mapinduzi kote nchini, watu walioangukia pua wakati wa kura
za maoni wameshikana uchawi na wenzao wakiwatuhumu kuwa ndiyo chanzo
cha anguko lao.
Akizungumza na gazeti hili, mmoja wa
maofisa wa Chama hicho Makao makuu, (jina linahifadhiwa kwa kuwa siyo
msemaji), aliyetakiwa kutoa tathmini ya zoezi hilo kuelekea Uchaguzi
Mkuu ujao, alisema wamepata malalamiko mengi kutoka kwa walioshindwa,
wakilalamikia kukiukwa kwa kanuni, rushwa, upendeleo na wizi.
“Kuna malalamiko mengi na chama hakiwezi
kukaa kimya, kitayafanyia kazi kwa kadiri inavyoweza ili washindi wawe
wameshinda kwa haki, watakaokutwa na hatia kwa mujibu wa taratibu zetu,
watashughulikiwa. Tunataka kuwahakikisha wana-CCM wote kuwa chama
hakiwezi kufumbia macho tuhuma dhidi ya yeyote,” alisema ofisa huyo.
Hadi gazeti hili linakwenda mitamboni,
mawaziri watano na wabunge wengi walikuwa wameanguka katika kura za
maoni, miongoni mwao wakiwa ni Waziri wa Mambo ya Ndani, Mathias
Chikawe, Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla, Naibu Waziri wa Mambo ya
Nje, Mahadhi Juma, Naibu Waziri Mambo ya Ndani, Pereira Silima na Waziri
wa Afya na Ustawi wa Jamii, Seif Rashid.
Kuanguka kwa mawaziri na wabunge hao
kumesababisha baadhi yao kuhama chama hicho kuelekea upinzani, huku
wakitoa tuhuma mbalimbali zinazoonyesha kutoridhishwa kwao na matokeo ya
kura hizo za maoni, ambazo hata hivyo, siyo muamuzi wa mwisho.

Note: Only a member of this blog may post a comment.