Hili ni tukio ambalo limechukua sana
headlines mitandaoni na kwenye Vyombo vya Habari vikubwa vya Kimataifa
Duniani, mtangazaji kavamiwa akiwa anarekodi show yake kwenye Kituo cha
Radio Brazil !!
Kinachoibua maswali kwa upande mwingine
ni kuhusu nani kahusika na mauaji hayo? wauaji waliingia mpaka ndani na
kuua alafu wakafanikiwa kutoka salama, mtangazaji Gleydson Carvalho kauawa kwa kupigwa Risasi tatu kichwani na kifuani.
Wauaji hao walivamia na kumzidi nguvu
mtu wa mapokezi, wakamkamata producer wa show akalazimishwa kuingia
chini ya meza… alafu wakamalizia kwa kumuua mtangazaji huyo ambaye
alikuwa maarufu sana kutokana na kuikosoa Serikali kushindwa kupambana
na tatizo la Rushwa.
Shuhudia video hiyo hapa....
‘Sikuwahi kufikiria kitu cha aina hii
kitakuja kutokea ndani ya nchi yetu… hili ni tukio linalostahili
Uchunguzi makini sana kufanywa na Serikali‘– amenukuliwa Marcos Coelho, Mwanasheria wa Mtangazaji huyo.

Note: Only a member of this blog may post a comment.