Gumzo kubwa kwa sasa nchini Tanzania, ni juu
ya mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa
John Pombe Magufuli!
Zipo
sifa nyingi ambazo ndiyo hasa zilizomfanya Magufuli awabwage makada
wenzake wa chama hicho na sifa hizohizo ndiyo zitakazowafanya Watanzania
wamchague kuingia ikulu kwenye uchaguzi mkuu.

Ndiyo, Watanzania wanategemea mtu atakayewavusha katika ‘bahari ya ufisadi’ kuelekea ‘nchi ya ahadi’ asiwe na madoa yanayohusu ufisadi wala matumizi mabaya ya madaraka. Magufuli ni msafi tofauti na wagombea wengine wa nafasi hiyo kutoka vyama vingine.
Ukija katika suala la uchapakazi, sote ni mashahidi wa jinsi alivyoziongoza vyema wizara zote alizowahi kuzitumikia sambamba na wananchi wake wa Chato.
Sote tumeshuhudia barabara nyingi ambazo kipindi cha nyuma zilikuwa hazipitiki katika majira yote ya mwaka hasa masika, zikijengwa kwa kiwango cha lami na kuwakwamua Watanzania wengi.
Pia amejitahidi kujenga madaraja yanayopitika majira yote ya mwaka sehemu mbalimbali za nchi hii. Ukijaribu kupima utendaji kazi wa mawaziri wengi, utagundua kwamba Magufuli anaweza kuwa anaongoza kwa kukamilisha miradi mingi chini ya wizara yake.
Kama Watanzania watataka kumchagua rais mchapakazi, asiye na hata chembe ya ubabaishaji, Magufuli pia atapeta.
Suala jingine linaloweza kuwa karata dume kwa Magufuli kuingia ikulu, ni uwajibikaji wake. Magufuli si kiongozi wa kukaa ofisini kama walivyo watendaji wengi wa serikali. Mara kwa mara tumekuwa tukimshuhudia akitembelea mwenyewe miradi mbalimbali chini ya wizara yake, wakati mwingine hata nyakati za usiku.
Magufuli si mtu wa kusubiri kuletewa ripoti bali huongoza kwa vitendo. Mara kadhaa amewatoa nishai wakandarasi wababaishaji ambao huidanganya serikali kwamba wamejenga miradi mbalimbali kwa kiwango kinachotakiwa kumbe nyuma ya pazia hufanya usanii.
“Mzee huwa anakwenda mwenyewe kukagua miradi, wakati mwingine bila hata kutoa taarifa, ghafla mnashtukia tu mheshimiwa huyo! Hata kama mlikuwa mnachakachua, ni lazima atawabamba kwa sababu anakuja bila taarifa, tunahitaji kiongozi wa namna hii,” Herman Massawe, mkazi wa Kinondoni jijini Dar es Salaam alimwambia mwandishi wa makala haya katika mahojiano ya kawaida.
Pamoja na sifa binafsi, Magufuli pia anabebwa na sifa ya chama chake kwa sababu ipo wazi kwamba CCM ndiyo chama pekee Tanzania kilichosambaa mpaka ngazi ya vijijini kabisa na kwenye maeneo mengine ambayo vyama vingine vya siasa havijafika.
Kwa msingi huo, endapo Watanzania wote watajitokeza na kupiga kura, hasa wale wa vijijini, ni dhahiri Magufuli atapata kura nyingi kuliko mgombea mwingine yeyote na hivyo kumrahisishia safari yake ya kuelekea ikulu na kuwatumikia Watanzania.
Tayari Magufuli ameshachukua fomu ya
kugombea urais sambamba na wagombea wa vyama vingine lakini kwa jinsi
upepo wa kisiasa ulivyo, inaonesha itakuwa rahisi zaidi kwake kuingia
ikulu kuliko mgombea mwingine yeyote kutokana na sifa alizonazo.
Mchakato wa kumpata mgombea mmoja kati
ya 38 waliokuwa wanawania nafasi ya kuteuliwa na CCM kushika nafasi
hiyo, haukuwa mwepesi hata kidogo. Sote tutakumbuka jinsi makada wengi
wakubwa walivyokuwa wakipigana vikumbo mjini Dodoma.
Mwisho, nyota ya jaha ikamuwakia
Magufuli ambapo mkutano wa chama hicho, ulimchagua kwa kishindo
kuipeperusha bendera ya CCM kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika
Oktoba 25, mwaka huu.
Tofauti na makada wengine waliokuwa
wakiwania nafasi hiyo ndani ya CCM, Magufuli hakuwa na kashfa wala
skendo hata moja, sifa ambayo kwa sasa ni nadra kuikuta kwa viongozi wa
nchi hii. Magufuli hajawahi kuhusishwa na kashfa yoyote ya matumizi
mabaya ya madaraka wala rushwa! CV yake ni safi kabisa katika kipengele
hicho.
Tanzania ya leo inahitaji kiongozi
ambaye si mla rushwa, mroho wa madaraka wala anayeendekeza vitendo
vilivyo kinyume na maadili ya uongozi na sheria za nchi. Endapo
Watanzania watazingatia kigezo hicho, Magufuli atapeta kwa kishindo!
Ndiyo, Watanzania wanategemea mtu atakayewavusha katika ‘bahari ya ufisadi’ kuelekea ‘nchi ya ahadi’ asiwe na madoa yanayohusu ufisadi wala matumizi mabaya ya madaraka. Magufuli ni msafi tofauti na wagombea wengine wa nafasi hiyo kutoka vyama vingine.
Ukija katika suala la uchapakazi, sote ni mashahidi wa jinsi alivyoziongoza vyema wizara zote alizowahi kuzitumikia sambamba na wananchi wake wa Chato.
Sote tumeshuhudia barabara nyingi ambazo kipindi cha nyuma zilikuwa hazipitiki katika majira yote ya mwaka hasa masika, zikijengwa kwa kiwango cha lami na kuwakwamua Watanzania wengi.
Pia amejitahidi kujenga madaraja yanayopitika majira yote ya mwaka sehemu mbalimbali za nchi hii. Ukijaribu kupima utendaji kazi wa mawaziri wengi, utagundua kwamba Magufuli anaweza kuwa anaongoza kwa kukamilisha miradi mingi chini ya wizara yake.
Kama Watanzania watataka kumchagua rais mchapakazi, asiye na hata chembe ya ubabaishaji, Magufuli pia atapeta.
Suala jingine linaloweza kuwa karata dume kwa Magufuli kuingia ikulu, ni uwajibikaji wake. Magufuli si kiongozi wa kukaa ofisini kama walivyo watendaji wengi wa serikali. Mara kwa mara tumekuwa tukimshuhudia akitembelea mwenyewe miradi mbalimbali chini ya wizara yake, wakati mwingine hata nyakati za usiku.
Magufuli si mtu wa kusubiri kuletewa ripoti bali huongoza kwa vitendo. Mara kadhaa amewatoa nishai wakandarasi wababaishaji ambao huidanganya serikali kwamba wamejenga miradi mbalimbali kwa kiwango kinachotakiwa kumbe nyuma ya pazia hufanya usanii.
“Mzee huwa anakwenda mwenyewe kukagua miradi, wakati mwingine bila hata kutoa taarifa, ghafla mnashtukia tu mheshimiwa huyo! Hata kama mlikuwa mnachakachua, ni lazima atawabamba kwa sababu anakuja bila taarifa, tunahitaji kiongozi wa namna hii,” Herman Massawe, mkazi wa Kinondoni jijini Dar es Salaam alimwambia mwandishi wa makala haya katika mahojiano ya kawaida.
Pamoja na sifa binafsi, Magufuli pia anabebwa na sifa ya chama chake kwa sababu ipo wazi kwamba CCM ndiyo chama pekee Tanzania kilichosambaa mpaka ngazi ya vijijini kabisa na kwenye maeneo mengine ambayo vyama vingine vya siasa havijafika.
Kwa msingi huo, endapo Watanzania wote watajitokeza na kupiga kura, hasa wale wa vijijini, ni dhahiri Magufuli atapata kura nyingi kuliko mgombea mwingine yeyote na hivyo kumrahisishia safari yake ya kuelekea ikulu na kuwatumikia Watanzania.

Note: Only a member of this blog may post a comment.