Thursday, August 20, 2015

Anonymous

NOMA SANA! Mtoto wa MCHEPUKO Ahatarisha Penzi la Ben KINYAIYA!

UCHUMBA wa muda mrefu wa Mtangazaji wa Runinga ya Clouds, Ben Kinyaiya na mpenzi wake, Suzy aishiye nchini Uingereza, umeingia shubiri baada ya msanii huyo kudaiwa ‘kuruka ngome’ na kupata mtoto na mwanamke mwingine aliyetajwa kwa jina moja la Nasra. 

Kwa mujibu wa chanzo cha habari hii, baada ya mwanamke wa Uingereza kung’amua juu ya uchafu wa Ben na mchepuko huo, aliamua ‘kumwaga ugali’ kwa kukata mawasiliano na Ben hali iliyomlazimu ‘presenta’ huyo ‘kudandia pipa’ hadi Uingereza kwa lengo la ‘kuzirudisha siku nyuma’. 

“Unajua Ben alikuwa na uhusiano na mwanamke mwingine hapa Bongo (Nasra) tofauti na huyo wa Uingereza (Suzy) na katika uhusiano wao, walipata mtoto wa kike anayeitwa Nilla na Suzy alipogundua hivyo, aliamua kukata uhusiano na Ben, hali iliyosababisha aende Uingereza kubembeleza,” kilisema chanzo.
Amani lilimvutia waya Ben ambaye alisema hataki kuingiliwa kwenye mambo yake binafsi.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.