Monday, August 3, 2015

Anonymous

Ni kweli SIMON MSUVA alidharau ushauri wa baba yake? Kaongea leo haya...

Mwanzoni mwa mwezi July kulikuwa na habari mbalimbali zilizoweka headlines katika mitandao ya kijamii kuhusu mchezaji wa Yanga Simon Msuva na baba yake Mzee Msuva, kila mtu alikuwa anazungumza kuhusiana na Simon Msuva.
August 3 Simon Msuva aliongea na millardayo.com na kuweka wazi kuhusiana na taarifa za yeye kupuuza ushauri wa baba yake, awali kulikuwa na uvumi kuwa baba yake Simon Msuva alimshauri aondoke Yanga na kwenda kutafuta changamoto sehemu nyingine hususani klabu ya Simba ambayo baba yake ndio klabu anayoipenda.
msuva
Msuva amezungumzia hizo taarifa za baba yake kutaka aondoke Yanga
“kiukweli Mzee anamapungufu yake siwezi kumuongelea sana sababu yeye sio mtu anayeniongelea mimi, mtu anayeniongelea mimi ni Management yangu ambayo inaweza ikaongea kila kitu kuhusu mimi”>>> Simon Msuva 
 
“kwa hiyo mzee anaweza ongea chochote kama mzazi, mzee kama mzee anaweza akawa kaongea ila watu wakamuelewa vingine. Mzee hawezi kuongea sitaki mwanangu acheze Yanga  aende nje au acheze Simba hicho kitu nakataa inawezekana waandishi labda wakawa wamemuuliza hivyo inategemea si unajua waandishi wanavyouliza “>>>Simon Msuva
IMGS6569

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.