Majambazi wamevamia daladala Ubungo Kariakoo maeneo ya Jangwani, mtu mmoja (abiria) aliyekuwa amebeba mfuko amepigwa risasi, watu kadhaa wamejeruhiwa. Majambazi haya yalikuwa na Pikipiki aina ya Boxer , kabla ya kupiga risasi walitaka abiria atoe hilo fuko la fedha yeye akagoma akiangalia kama atapata msaada kutoka kwa abiria ndipo walimwambia dereva kusimama na kutwanga risasi huyo abiria akaachia fuko linalosemekana kuna fedha, haijajulikana ni fedha au ni dhahabu/Tanzanite maana abiria alikuwa hawezi tena kuongea.
Taarifa kamili zitawajia www.kandiliyetu.com hapa hapa!
Taarifa kamili zitawajia www.kandiliyetu.com hapa hapa!


Note: Only a member of this blog may post a comment.