Diva wa R&B asiyekaukiwa vituko kutoka nchini Marekani, Robyn Rihanna Fenty ‘RiRi’.
New York, Marekani
DIVA wa R&B asiyekaukiwa vituko kutoka nchini Marekani, Robyn Rihanna Fenty ‘RiRi’ hivi karibuni amekuja juu baada ya staa wa NBA, Matt Barnes kudai kuwa kwa sasa wapo karibu na ikiwa mipango yao itakwenda vizuri, siku si nyingi wanaweza kudumbukia kwenye dimbwi la malavidavi kulifufua upya penzi lao.
Kwa upande wake RiRi, baada ya kuzinyaka ‘drama’ hizo zilizokuwa zinaendelea kwenye mitandao ya kijamii alikanusha madai hayo kwa kutupia kipande cha video kwenye ukurasa wake wa Instagram kinachoonesha mahojiano kati ya Matt na kituo fulani cha habari kisha akaambatanisha maandishi yaliyokanusha madai hayo. “Shetani muongo, hakuna kinachoendelea kati yetu, hakuna lolote,” aliandikaRihanna.

Note: Only a member of this blog may post a comment.