Bahati Bukuku.
Brighton Masalu
MWIMBAJI wa nyimbo za Injili, Bahati Lusako Bukuku amefungukia kuridhika na maisha yake bila mume kwamba suala la kuwa naye halina utashi wala ulazima na kuongeza kuwa ni vyema kama jambo limeshindikana kuachana nalo.
MWIMBAJI wa nyimbo za Injili, Bahati Lusako Bukuku amefungukia kuridhika na maisha yake bila mume kwamba suala la kuwa naye halina utashi wala ulazima na kuongeza kuwa ni vyema kama jambo limeshindikana kuachana nalo.
Akichezesha mdomo na Amani, Bukuku alisema watu wamekuwa na tafsiri
batili juu yake, kutokana na kuishi muda mrefu pasip-okuwa na ndoa, huku
akiweka wazi kuwa maisha hujengwa na mwenye maisha na kufafanua kwamba
anaridhika na maisha hayo na wala siyo dhambi kuishi peke yake.
“Watu wanashindwa kusoma na kuielewa vyema Biblia, suala la ndoa halina mashiko wala amri ya kwamba usipofanya itakuwa ni dhambi, ndiyo maana hata Mtume Paulo katika nyaraka zake kwa Wakorintho, alilifafanua sana jambo hilo, ” alisema Bahati.
“Watu wanashindwa kusoma na kuielewa vyema Biblia, suala la ndoa halina mashiko wala amri ya kwamba usipofanya itakuwa ni dhambi, ndiyo maana hata Mtume Paulo katika nyaraka zake kwa Wakorintho, alilifafanua sana jambo hilo, ” alisema Bahati.

Note: Only a member of this blog may post a comment.