Wednesday, August 5, 2015

Anonymous

Michezo Cannavaro kazungumzia uhamisho wake ulikwama wapi wa kujiunga na Al Ahly ya Misri.

Nahodha wa Dar Es Salaam Young African pamoja na timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars Nadir Haroub Cannavaro amezungumzia kuhusiana na zile taarifa za yeye kuhitajika na klabu ya Al Ahly ya Misri ambazo ziliishia kimya kimya. Cannavaro alihusishwa kujiunga na klabu ya Al Ahly baada ya kuonekana uwezo wake kwenye mechi ya Yanga dhidi ya Al Ahly.
Ngao
Cannavaro uwezo wake ulionekana katika mchezo wa pili wa marudiano uliochezwa mwanzoni mwa mwaka 2014 Misri ambapo Yanga ilifungwa goli 1-0 nakulazimika kwenda katika hatua ya mikwaju ya penati baada ya ule mchezo wa awali uliopigwa Dar Es Salaam kumalizika kwa Yanga kushinda goli 1-0.
cannavaro-FILEminimizer
Cannavaro kama mmoja wa watu walioonyesha uwezo mzuri katika dakika zote 90 na hata katika hatua ya mikwaju ya penati uwezo wake uliwavutia viongozi wa Al Ahly ya Misri kiasi kwamba walienda hadi hotel waliofikia Yanga na kuongea na kiongozi wa Yanga.
NORDIN HAROUB-YANGA-300
“Ilikuwa ni kweli ila uongozi wetu sisi na Al Ahly kidogo ulikuwa sio mzuri kutokana na yule kocha alitufuata hotelini na aliongea na Vice president wetu na baada ya hapo mazungumzo yalikuwa yameenda vizuri ila yule kocha alifukuzwa Al Ahly ndio maana ikawa kidogo  imekatika ila tu maendeleo yalikuwa mazuri sana kutokana kwamba Yanga walikuwa wanahitaji milioni 200 kama sikosei”>>> Cannavaro
Nikukumbushe tu mdau wangu ilivyokuwa katika mchezo na penati ya Cannavaro katika video hiyo hao chini!

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.