Simon Msuva ni winga mshambuliaji wa klabu ya Dar Es Salaam Young African ambae msimu uliomalizika aliibuka kuwa mfungaji wa bora wa Ligi Kuu Tanzania bara katika msimu uliomalizika wa mwaka 2014/2015. Awali kulikuwa na taarifa za Simon Msuva kwenda kufanya majaribio pasipo ridhaa ya viongozi wa Yanga.
Msuva alipata
nafasi ya kuongea na timu ya millardayo.com na kuelezea namna ya safari
yake ya kwenda Afrika ya Kusini kufanya majaribio katika klabu ya Bidvest Wits FC ilivyokuwa.
“In short
ilikuwa hivi ile timu ilileta ofa lakini ile ofa waliileta katika
mazingira ambayo Yanga hawakuwa wamerizika waliona kama imeletwa
kihuni, nazungumzia kihuni kwa sababu haikufika kwa Uongozi moja kwa
moja ilikuja ila ikawa imefahamika kuwa Simon anatakiwa kwenda katika
timu akafanye majaribio ili yule kocha aweze kumchukua katika timu
nikaletewa tiketi”

Simon Msuva akiwa Afrika Kusini kwa ajili ya majaribio
Simon Msuva akiwa Afrika Kusini kwa ajili ya majaribio
“Kabla
sijaondoka siku mbili mbele nikawaambia viongozi, wakaniambia kwamba
Simon huwezi kuondoka bado kuna mechi mbili ya Azam FC na Ndanda, ila
nikawaambia ubingwa tushatangaza ila wakagoma na mimi unahitajika South
kabla ya Ligi haijaisha ila kocha akanikubali baadae dau walilokuwa
wanataka Yanga na wale wakawa wameshindwana”

Note: Only a member of this blog may post a comment.