Tuesday, August 18, 2015

Anonymous

MENINAH ameolewa ghafla, Soudy Brown kampata kaka yake..Kumbe mipango ilikuwa hivi !! (U Heard)

Soudy Brown huwa anazinasa stori za chinichini, anachokifanya ni kuwatafuta wahusika na kucheki nao kama kwenye hizo za chinichini zina ukweli au ni za kuzushwa, iliyomfikia jamaa leo inahusu ishu ya staa wa Muziki Meninah la Diva kuolewa. 

Gossip Cop akaamua kumcheki kaka wa Meninah kwa sababu Meninah mwenyewe yuko honeymoon.. kaka amesema ndoa ilikuwa ya ghafla na kila kitu walikisimamia wenyewe kama Familia, hakukuwa na michango yoyote iliyokusanywa ili kufanikisha… ndoa ya Meninah na mtoto na Waziri wa zamani wa Nishati na Madini, Prof. Muhongo imefanyika Jumapili nyumbani kwa akina Meninah, Kigamboni Dar. 

Muziki je anauachaje? Kaka wa Meninah amesema japo dada yake kaolewa lakini ataendelea kufanya muziki lakini kutakuwa na mabadiliko kidogo tu kwenye aina ya muziki atakaoufanya.
U Heard iko kwenye hii sauti pia mdau wangu.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.