Thursday, August 20, 2015

Anonymous

Maskini Mke wa TYSON...Akumbana na MAMBO MAZITO Bongo Movies! Badilikeni Jamani!

bitewatyson3ALIYEKUWA mke wa muandaaji mahiri wa filamu Bongo George Tyson, ambaye kwa sasa amejikita kwenye ulimwengu wa filamu, Beatrice Shayo amesema kuwa, anajuta kuingia kwenye tasnia hiyo kutokana na kutawaliwa na imani za kishirikina. 

Akipiga stori na Amani, Beatrice alisema awali alikuwa akiyasikia tu hayo mambo pasipo kujua undani wake, baada ya kujikita kwenye tasnia hiyo ndipo akakumbana na mambo mazito tofauti na jinsi alivyojiweka kwa kupenda maombi muda wote, sababu alishangazwa na kitendo cha wasanii wenziye kumlazimisha kufanya ndumba.

“Sanaa yetu imetawaliwa na mambo ya ajabu sikuwahi kuwaza kama hivi vitu vipo jamani, mbali na rushwa ya ngono hayo ya kurogana ndiyo usiulize, kuna watu wanaenda kwa waganga kuwashusha nyota wenzao, isitoshe kuna wakati nilikuwa naenda kambini kucheza movie ambayo nilipewa dili na msanii mkubwa tu, sasa wenzangu ambao wengine ni mastaa kabisa (aligoma kuwataja majina) wakaanza kunilazimisha kwamba ili niwini katika sanaa ni lazima nifanye mambo ya ushirikina vitu ambavyo sipendi hata kuvisikia nikajikuta nakosa raha,” alisema.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.