Msanii
wa Bongofleva Nay wa Mitego ambaye kwa sasa anafanya poa na wimbo wake
wa ‘Sina Muda’ amefunguka na kutoa somo kwa wanaume kwa kuwataka
kutowapiga wanawake wao pindi wanapowakosea au wanapotofautiana kutokana
na mambo mbalimbali katika maisha ya kila siku.
“Ujanja wangu wote, ukorofi, ubabe lakini sijawai kumpiga mwanamke hata siku moja. Hata uwe umenikosea kiasi gani, nishawahi kumfumania mwanamke wangu akiwa na mwanaume ndani na sikumfanya chochote nilichukua kilicho muhimu nikasepa. Kumpiga mwanamke siyo solution akikushinda mwanamke mwambie wasalimie nyumbani, unatafuta mkali kuliko yeye sababu wapo wengi,” alisema Nay wa Mitego.
Nay wa Mitego alishawahi kuimba wimbo maalum ambao alikuwa akihamasisha wanaume kutowapiga wanawake katika maisha ya kawaida lakini pia msanii huyo anasema anachukia sana na hapendi kuona mwanamke akinyanyaswa kwa kupigwa hata kama kweli atakuwa wamefanya kosa, kwa kuwa anaamini makosa yanaweza kusahihishwa kwa njia mbalimbali tofauti na kipigo.


Note: Only a member of this blog may post a comment.