Saturday, August 15, 2015

Anonymous

Hans van Der Pluijm, Nsajigwa watoa kali Mbeya

pluijmHans van Der Pluijm
Derick Lwasye, Mbeya
MECHI kati ya Yanga na Tanzania Prisons iliyochezwa juzi kwenye Uwanja wa Sokoine, mbali na kutawaliwa na ubabe, ilisababisha kituko ambacho kilihusisha makocha wa Yanga.

Mechi hiyo ambayo ilitawaliwa na ubabe kwa wachezaji wa timu zote kucheza kibabe kama vile ni mechi ya ushindani, ilishuhudia Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm na msaidizi wake, Shadrack Nsajigwa, wakiingia uwanjani baada ya mchezaji wao kuchezewa faulo.

Wachezaji wa timu zote walionekana kuwa na presha kubwa kutokana na mchezo huo kuwa wa kasi huku wale wa Prisons wakiwa ndiyo wa kwanza kuonyesha kuja juu kutokana na kufungwa mabao 2-0.

Kabla ya tukio hilo la makocha hao kuingia uwanjani, beki wa kushoto wa Yanga, Haji Mwinyi na Zani Kufo wa Prisons walitolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kuchapana makonde kavukavu.

Katika dakika ya 67, Pluijm na Nsajigwa ambaye amepewa jukumu hilo kutokana na Charles Mkwasa kuwa bize na Taifa Stars, walivamia uwanja baada ya kiungo wao, Deus Kaseke kuchezewa rafu na James Mwasote.

Mara baada ya tukio hilo la rafu, kulitokea vurugu baina ya pande mbili huku beki wa Yanga, Mbuyu Twite naye akitibuana na Lambart Sabianka wa Prisons, kuona hivyo ndipo makocha hao wakaingia mpaka uwanjani wakati mchezo ukiendelea ili kutuliza presha, jambo ambalo walifanikiwa.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.