WATANYOOKA tu! Hiyo
ndiyo kauli waliyoitoa wafuasi wa CCM jijini Dar baada ya Katibu Mkuu wa
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Willibrod Slaa na
Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (Cuf), Ibrahim Lipumba kujiweka pembeni
katika shughuli za Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
Slaa amedaiwa kujichimbia nyumbani kwake
Mbweni jijini Dar na kukataa kuzungumzia hatma yake kisiasa na kuacha
shughuli za Ukawa zikiendelea bila uwepo wake huku Agosti 6, mwaka huu,
Lipumba akijitokeza hadharani na kutangaza kujivua wadhifa wake akidai
kwa kile alichodai kukiukwa kwa makubaliano ya awali ya umoja huo.
Mara baada ya vigogo hao kujiweka
pembeni, wanachama mbalimbali wa CCM walizungumza na Risasi Jumamosi na
kueleza hisia zao juu ya viongozi hao na kusema kujitoa kwao ni ishara
nzuri ya umoja huo kusambaratika.
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dr. Willibrod Slaa.
“Ukawa watanyooka tu. Sisi tulijua
zamani kwamba safari yao waliyoianzisha haiwezi kufanikiwa, ona sasa
Slaa ameshajiweka pembeni, hashiriki vikao vya Ukawa, Lipumba naye ndiyo
huyo ameshajivua uongozi.
“Sasa kama mwenyekiti wa chama anajivua
uongozi ikiwa imebaki miezi miwili tu kuelekea uchaguzi kuna nini hapo?
Tayari wamekaa, CCM ushindi mapemaaa,” alisema Gilbert, mkazi wa Sinza
jijini Dar.
Kama hiyo haitoshi, Mary wa Ubungo jijini Dar, alisema:
“Ukawa wanaangukia pua. Siku si nyingi tutasikia wametibuana na kurejea kulekule kwa kila chama kusimamisha mgombea wake.”

Note: Only a member of this blog may post a comment.