Sunday, August 2, 2015

Anonymous

BREAKING NEWS: Aliyekuwa Mkuu wa Idara ya Ujasusi na Rafiki Mkubwa wa Nkurunziza wa Burundi Auawa Leo!

le-chef-des-imbonerakure
Jenerali Adolphe Nshimirimana.
ALIYEKUWA Mkuu wa Idara ya Ujasusi nchini Burundi na mtu wa karibu wa Rais Pierre Nkurunziza, Jenerali Adolphe Nshimirimana ameuawa katika shambulizi la roketi akiwa kwenye gari lake kaskazini mwa Mji wa Bujumbura leo.
Nkurunziza_0
Imeripotiwa kuwa Jenerali Adolphe ameuawa pamoja na walinzi wake watatu katika shambulio hilo.
Jenerali Adolphe Nshimirimana alikuwa rafiki wa karibu wa rais Pierre Nkurunziza hata baada ya kuondolewa madarakani kama Mkuu wa Idara ya Ujasusi mwezi Novemba mwaka jana.
Nshimirimana alituhumiwa kwa kusimamia oparesheni za kukabiliana na waandamanaji baada ya Rais Nkurunziza kutangaza kwamba atawania muhula wa tatu mbali na kuhusika pia katika kuzima jaribio la mapinduzi dhidi ya rais huyo.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.