Wednesday, August 26, 2015

Anonymous

40 ya Mtoto wa SANDRA wa Bongo Movies Kivutio!

SANDRA27.jpg
Imelda Mtema
SHEREHE ya kutimiza siku 40 tangu azaliwe mtoto wa msanii nyota wa Bongo Movies, Salama Salmini ‘Sandra’ aitwaye Khaliam zilikuwa kivutio baada ya kuhudhuriwa na mastaa na watu mbalimbali ilipofanyika nyumbani kwa wazazi wa msanii huyo, Tegeta Kibaoni, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
 

Katika shughuli hiyo, vyakula na vinywaji vya aina mbalimbali viliandaliwa, ambapo pia ndugu, jamaa na majirani walifurahishwa kwa kuwaona mastaa wa fani tofauti waliokuwa wamealikwa.
Baadhi ya wasanii waliohudhuria katika sherehe hiyo alikuwa ni Salome Urassa ‘Thea,’ Halima Yahaya ‘Davina,’ Jennifer Kyaka ‘Odama,’ Sabrina Rupia ‘Cathy,’ Mama Loraa, Herieth Chumila na wengine wengi .

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.