Wednesday, July 15, 2015

Anonymous

ZARI WA LEO, WA KESHO....DIAMOND AFUNGUKA!

10843996_788400007864260_370710352_n
Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’,  na mwandani wake, Zarinah Hassan ‘Zari the Boss Lady’
Musa Mateja
Siku za kujifungua za mwandani wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari the Boss Lady’ sasa zinahesabika.
Habari kutoka kwa chanzo chetu ndani ya Wasafi Classic Baby (WCB) kimelieleza gazeti hili kwamba, kwa sasa mwanadada huyo ‘amechoka’ ambapo anatarajiwa kujifungua mwishoni mwa mwezi huu au mwanzoni mwa mwezi ujao.
malovee2“Kama siyo mwishoni mwa mwezi huu, basi itakuwa mwezi ujao maana kwa muonekano tu mama kijacho (Zari) amechoka ndiyo maana hatembei sana na Diamond.
“Kwa sasa yupo Sauzi (Afrika Kusini) na hatuna uhakika sana kama ataweza kuhudhuria utoaji wa Tuzo za MTV Music (Mama) wikiendi ijayo,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:
“Diamond mwenyewe amekuwa akimuomba sana Mungu amjalie bibiye ajifungue salama.” 

Kwa upande wake Diamond alikiri kwamba ni kweli Zari atajifungua muda wowote kuanzia sasa.

“Ni kweli siku zinahesabika. Kama siyo mwezi huu mwishoni, basi itakuwa mwezi ujao,” alisema Diamond.
Kwa sasa Diamond yupo kwenye presha kubwa ya kuomba mashabiki wake wampigie kura kwa wingi katika Tuzo za MTV Music (Mama) baada ya kuteuliwa kuwania Vipengele vya Msanii Bora wa Kiume Afrika, Mtumbuizaji Bora wa Kiume Afrika na Nyimbo Bora ya Kushirikiana Afrika.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.