Thursday, July 2, 2015

Anonymous

VIOJA UCHAGUZI CCM 2015

IMG_9960 Staa wa Bongo movie, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ akisalimiana na makada waliofika kwenye mkutano wake wa kutangaza nia ya kugombea ubunge jimbo la Kinondoni kwa tiketi ya CCM.
Musa Mateja
WAKATI vioja vya kuelekea uchaguzi mkuu vikiendelea huku wagombea wa nafasi mbalimbali wakikazana kutangaza nia, mambo hayakuwa mazuri kwa Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ alipokuwa akitangaza nia ya kugombea ubunge wa Kinondoni baada ya mkutano wake kuvunjika kabla hajamaliza, Amani lina stori kamili.
Tukio hilo lilijiri Jumapili iliyopita katika Mtaa wa Bwawani, Kinondoni ambapo Steve Nyerere aliandaa mkutano huo ambao awali aliuita wa kuhamasisha watu kujiandikisha katika daftari wa wapiga kura.
2…Steve Nyerere na makada alioongozana nao wakiondoka eneo ambapo mkutano huo ulipangwa kufanyika, ni baada ya kuahirishwa kwa mkutano huo.
Wakati Steve Nyerere akijinadi kuwa anataka Kinondoni yenye mabadiliko katika kila sekta na kuhamasisha watu wamchague, ghafla aliibuka Mwenyekiti wa Mtaa wa Bwawani, Omar Karembo akamnyang’anya kipaza sauti na kusema:
IMG_9963“Jamani tusikilizane. Hapa kuna mapaparazi na wadau mbalimbali wameshaanza kusambaziana taarifa. Kuna vitu inabidi viende kwa utaratibu na kwa faida ya Steve inabidi niuvunje huu mkutano.”
Baada ya tamko hilo, vurugu za hapa na pale ziliibuka ambapo watu walihoji kwa nini mwenyekiti huyo aliuvunja mkutano pasipo kuanika sababu. Steve Nyerere alisaidiwa na baunsa kutoka jukwaani akionesha dalili za kutaka kulia huku mwenyekiti huyo akitokomea zake.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.