Monday, July 13, 2015

Anonymous

NGOMA wa YANGA SC Mtampenda Tu

Mshambuliaji mpya wa Yanga ,Mzimbabwe Donald Ngoma.
Na Khadija Mngwai Dar es Salaam
Mshambuliaji ambaye alishika nafasi ya pili kwa ufungaji msimu uliopita, Amissi Tambwe aliifungia timu yake bao la pili dakika tano tu baadaye na kuwafanya mashabiki wa timu hiyo walipuke kwa furaha. 

Hata hivyo, Ngoma alifunga bao lake dakika kumi tu baada ya Malimi Busungu kutoka na nafasi yake kuchukuliwa na Kpah Sherman, hali ambayo inaonyesha kuwa kombinesheni yao itakuwa hatari sana msimu ujao.
“Tatizo la timu yangu ni kombinesheni kwa sasa, tunatakiwa kwenda kwenye michuano ya Kagame tukiwa sawa, lakini naona kama vile bado wachezaji wangu hawajaelewana vizuri,” alisema Kocha wa Yanga, Hans van Pluijm. 

Kwa upande mwingine, straika a zamani wa Yanga, Mkenya Boniface Ambani, aliyekuwa uwanjani jana, amempigia saluti Ngoma, akisema ni bonge la straika ambaye atafanya makubwa Bongo. 

“Ana uwezo mkubwa wa kufunga mabao. Nafurahia kasi yake ya kukimbia na mpira na kumiliki kwa kifua. Aina ya uchezaji wake inaendana na soka la Tanzania, naamini atafunga mabao mengi tu,” alisema Ambani.
Imeandikwa na: Mohammed Mdose, Wilbert Molandi, Hans Mloli na Sweetbert Lukonge

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.