Mgombea Ubunge Jimbo la Njombe Kusini, Rose Mayemba ambaye anagombea Jimbo ambalo lilikuwa la Spika Anne Makinda(Pichani juu) juzi alimkuta nyoka amejiviringisha kwenye siti ya abiria kwenye gari yake wakati akiwa Hotelini Njombe.
Nyoka huyo alikutwa kwenye siti kama
abiria anayesubiri dereva aingie awashe gari waondoke, Mbunge huyo
alikuwa kwenye Hoteli ambayo walikutana na Viongozi wa CHADEMA.
Mayemba ambaye ni
Mtunza Takwimu Mkuu wa CHADEMA Wilaya ya Njombe alisema baada ya kuingia
kwenye gari yake aina ya RAV 4 alishangaa kuona kitu kimejiviringisha
kwenye siti ya mbele.
“Nilipokiona hicho kitu wazo la haraka
nikajua ni mkanda wa abiria ambaye nilikuwa nimembeba ameusahau…
nilipoona ni nyoka anataka kujiviringisha mkononi nilitoka mbio kwenda
kuwaita wenzangu” >>> Rose Mayemba.
Mgombea Ubunge huyo amesema hajui nyoka
aliingiaje kwenye gari lake na hawezi kumlaumu mtu ila safari yake
Bungeni anamtegemea zaidi MUNGU na hatishiki na chochote.


Note: Only a member of this blog may post a comment.