Friday, May 1, 2015

Anonymous

SUMAYE: CCM INAJIKAANGA KWA MAFUTA YAKE

Waziri Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye, amesema Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinaweza kujikaanga kwa mafuta yake, iwapo kitachelewa kutangaza mgombea urais katika kinyang’anyiro cha Uchaguzi mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu. 

Sumaye alisema hayo baada ya kuombwa na waandishi wa habari mjini hapa, wakimtaka azungumzie hali ya kisasa nchini, uchaguzi mkuu ndani ya CCM na hali ya utekelezaji wa adhabu ya kifo dhidi ya watu waliohukumiwa kunyongwa hadi kufa. 

Alisema wengi wana shauku ya kufahamu atakayepeperusha bendera ya CCM kugombea urais, hiyo ikiwa ni kutokana na kupewa nafasi kubwa ya kushinda uchaguzi huo, na kwamba katika hali isiyo ya kawaida kimechelewa kumtaja.
“Anapotangazwa mapema watu wanatafiti, kufahamu ubora wake na kuwa na msimamo wa kumchagua, hata mgombea anapata muda wa kutosha kufikiri na kufanya kampeni za kutosha,” alieleza. 

Alisema pia hiyo itasaidia wapinzani kukosa muda wa kutosha kumshambulia mgombea anapotangazwa kwa kuchelewa, hata yeye mgombea anaathiriwa kwa kutopata muda wa kutosha kufanya kampeni. 

Wananchi nao hawapati muda wa kutosha kutafiti ili kufahamu ubora wake, ikiwa ni pamoja na kumhoji maswali, ili wasifanye uchaguzi kwa kufuata mkumbo.
“Hata mimi hali hii sijaielewa, katika hali ya kawaida sasa hivi wenye nia ya kugombea wangeshachukua fomu na kuingia mikoani kutafuta wadhamini, kwa mfano, uchaguzi wa mwaka 2005, mgombea alitangazwa Mei 05,Sumaye, 

Sumaye alisema anaamini siku siyo nyingi ratiba ya wenye nia ya kuwakilisha chama katika kugombea urais, ubunge na udiwani itatolewa na chama hicho.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.