Friday, May 1, 2015

Anonymous

D’BANJ AJIGONGA KWA MPENZI WA ZAMANI!

Mwanamuziki kutoka Nigeria D’ Banj.
INAVYOONEKANA bado mwanamuziki D’ Banj analo penzi la kweli kwa mpenzi wake wa zamani, Adama Indimi baada ya juzikati kujigonga kwake kwa kumtumia ujumbe mzuri mama wa demu huyo katika siku yake ya kuzaliwa.
Aliyekuwa mpenzi wa mwanamuziki D’ Banj Adama Indimi.
Jamaa alifanya hivyo kupitia mtandao wa Instagram ambapo mbali na kumtakia heri ya kuzaliwa, pia alimuelezea mama huyo kama mkarimu na mpenda watu. 

Achilia mbali hilo, D’ Banj pia akaposti ujumbe mwingine, safari hii akiuelekeza kwa dada wa Adama, Meran Indimi aliyetimiza miaka 25 juzi ambapo naye alimuelezea kama mrembo na sapota wake namba moja.
Meseji hizo zilitafsiriwa kuwa ni kama jamaa anajigonga kwa Adama na amejaribu kufikisha ujumbe kupitia ndugu zake.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.