Friday, May 1, 2015

Anonymous

Mheshimiwa Mbunge wa Dimani (CCM) Apewa Adhabu Hii na Mahakama Baada ya Kumtelekeza Mtoto!


Hawa Kundani (mwenye vazi jeusi), anayedai kuzaa na kutelekelezwa na mbunge wa Dimani, Abdallah Sharia Ameir, akiwa chini ya ulinzi wa polisi baada ya kuvamia kikao cha Kamati ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala kilichokuwa kikifanyika Dar es Salaam siku zilizopita. 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemuamuru Mbunge wa Jimbo la Dimani Zanzibar, Abdallah Sharia Ameir (CCM) kutoa Sh 200,000 kila mwezi kwa ajili ya matunzo ya mtoto wake wa kiume, mwenye umri wa miaka mitatu na nusu, anayedaiwa kumtelekeza. 

Pamoja na amri hiyo, Hakimu Mkazi, Hellen Liwa alisema mbunge huyo atatoa kiasi hicho cha fedha kuanzia siku alipokoma kutoa matunzo na matibabu kwa mtoto huyo, anayetajwa kuwa ni mlemavu.

Pia, aliamuru mtoto huyo kulelewa na wazazi wake na siyo bibi yake, kama alivyokuwa akitaka mbunge huyo. Hivyo ataendelea kukaa na mama yake.
Kwa upande wake, Wakili Gideon Mandes aliyekuwa akimtetea Hawa Deus aliyekuwa mke wa mbunge huyo, alisema kupitia hukumu hiyo Mahakama imetoa uamuzi wa haki.
“Kupitia hukumu hii nimebaini wazazi wanawajibu wa kumtunza mtoto wanayemzaa bila ya kujali hali yake hata kama ni ya ulemavu asitelekezwe na imedhihirisha hakuna mtu aliye juu ya sheria na kwamba sheria ipo sawa kwa kila mtu,”. 

Wakili huyo aliwashauri Watanzania wenye matatizo na changamoto kama hizo, kuweka bidii ya kuijua sheria na taratibu zake ili waweze kuitumia kupata haki na suluhisho kupitia Mahakama.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.