Davido.
STAA wa muziki kutoka nchini Nigeria, Davido ametupia mtandaoni picha ya mjengo wake mpya uliopo huko Atlanta nchini Marekani.
Davido ambaye anajiandaa kuachia albamu yake ya pili, alitupia picha hizo kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram jana.
Staa huyo bado yupo nchini Marekani na kupitia picha hizo aliandika kuwa mtoto wake wa kike atakuwa na chumba chake kikubwa ndani ya mjengo huo unaodaiwa kununuliwa kwa Naila za Kinigeria milioni 33.
Katikati mwa mwezi huu, staa huyo alifanikiwa kupata mtoto wake wa kwanza ambaye ni wa kike na mama wa mtoto huyo ni Sophie Momodu.

Note: Only a member of this blog may post a comment.