
Mkutano huo umehudhuriwa na viongozi wengi wa Chama cha Mapinduzi akiwemo mwanasiasa Mkongwe nchini Kingunge Ngombare Mwiru ambaye alipopata machache ya kuongea alisema nchi sasa inahitaji Kiongozi kama Edward Lowassa.
Akimuelezea Lowassa, Kingunge amesema kuwa Lowassa ni mtu ambaye amelelewa ndani ya chama na kupata misingi yote ya maadili ya kitanzani na ya CCM, pia ni miongoni mwa viongozi ambao walipitia utaratibu wa chama wa kupitia jeshini akiwa pamoja na Kikwete, Kinana n.k
Mwisho mzee Kingunge amesema kwa niaba ya wazee ndani ya chama, anamuunga mkono Lowassa na kumshauri yeye pamoja na makada wengine kusameheana kwa lolote ambalo wamekoseana.
"Hata sisi zamani ilikuwa tukikanyagana tunayaacha na tunasonga mbele, safari ya matumaini ndiyo imeanza, mpaka kieleweke" Amesema Kingunge


"Hata sisi zamani ilikuwa tukikanyagana tunayaacha na tunasonga mbele, safari ya matumaini ndiyo imeanza, mpaka kieleweke" Amesema Kingunge


Note: Only a member of this blog may post a comment.