Keisha aliliambia gazeti la Mtanzania kuwa, sababu kubwa inayomfanya asitamani kuongeza mtoto kwa sasa ni kutokana na kuwa na watoto wawili wa kiume wenye umri mdogo.
“Najua watu wengi wanapenda watoto na hata mashabiki wangu wanatamani sana niendelee kuzaa, kiukweli bado nahitaji kulea madume yangu, kwani umri wao bado ni mdogo sana,” alisema Keisha.
Mtoto wa kwanza wa msanii huyo ana miaka minne na wa pili ana mwaka mmoja.
“Kama nitabeba ujauzito mwingine kwa sasa mimi na baba yao tutakuwa hatuwatendei haki hawa watoto wetu, wanahitaji muda wa kukua zaidi ndipo tufikirie kuongeza wenzao wengine,” alisema Keisha.

Note: Only a member of this blog may post a comment.