Ingawa hatuko nae duniani lakini upendo wake pamoja na nyimbo zake
bado upo kwenye hizia za wengi na ndio maana jina lake ni gumu
kusahaulika miongoni mwetu, alikua rapper kwenye game ya bongofleva
ambaye hakuwahi kuchokwa, namzungumzia marehemu Albert Mangweha.
Wakati muziki wa kizazi kipya unaanza ilikua ni nadra sana kukuta
wazazi wakiwasupport watoto wao waliokuwa wakifanya muziki huo kwa
kipindi hicho kwa sababu asilimia kubwa ya wazazi walikua
wakiamini muziki huu ni wa kihuni.

Mama Mangwea
Mama Mangwea
Kwenye hii post leo tuko na Mama mzazi wa Ngwea na anataja nyimbo zinazomvutia na anazozikumbuka kutoka kwa Ngwea, anasema >>’Naipenda She Got a Gwan
kwa sababu inaonyesha upendo halisi jinsi mtu akiwa na mwenzi wake
waone kuna hali ya kusameheana au kuchukuliana katika upendo na ndiyo
maisha yanayoweza kuwa katika watu wawili wanapokua pamoja‘
‘Nilianza kuusikia kwenye radio
baadae akaja hapa tukaongea nae tukamwambia wimbo wako kweli Noma
umetoka vizuri akacheka kwa sababu yeye alikua mtu wa kucheka,ukimwambia
kitu cha kufurahisha anacheka anasema poa tu mama‘

Note: Only a member of this blog may post a comment.