Wednesday, May 27, 2015

Anonymous

JUSTIN BIEBER ATAFUTA MWANAMKE WA KUOA!

UNAWEZA kusema sasa Justin Bieber amekuwa hii ni baada ya kutamka wazi kuwa anahitaji mwanamke ambaye anajiamini na mwaminifu ili aweza kuishi naye katika maisha yake baadaye.
Justin Bieber akiwa na rafiki yake Jayde Pierce.
Hii ni kutokana na star huyo kuwa karibu na mwamitindo Jayde Pierce (19)  ambaye hivi karibuni  wamekuwa wakiongozana na haifahamiki kama ni wapenzi au la. Japo hakuna aliyeweka wazi uhusiano huo lakini inaelezwa kuwa wawili hao wamekuwa wakikutwa sehemu mbalimbali pamoja ikiwemo kwenye migahawa. 

Kabla ya kuwa na Jayde, Bieber alikuwa akihusishwa kutoka na Haley Baldwin baada ya kuachana na mpenzi wake wa awali Selena Gomez.“ Nahitaji mtu ambaye anajiamini na mwaminifu, nahitaji kutafuta msichana anayevutia na ambaye atakuwa na mimi maisha yangu yote. “ Nataka  uhusiano salama na  watu wasiweze kunizungumzia,”.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.