Thursday, May 28, 2015

Anonymous

AIBU TUPU: ISABELLA ANASWA NA MCHEPUKO AKIDENDEKA LIVE MUDA MFUPI KABLA YA KUVISHWA PETE NA LUTENI KARAMA!

Issa mnally  
AMA kweli duniani kuna mambo! Mdada anayehangaika kutafuta jina katika tasnia ya muziki wa Kibongo, Isabella Mpanda ‘Bella’ aliitia doa sherehe yake ya kuvishwa pete ya uchumba baada ya kunaswa akidendeka na mchepuko dakika chache kabla ya tukio hilo muhimu.

Mbongo Fleva Masoud Karama ‘Luteni Kalama’ akimvisha pete mpenzi wake wa kitambo, Isabella Mpanda ‘Bella’.
Msanii huyo  alivishwa pete na mpenzi wake wa kitambo, Mbongo Fleva Masoud Karama ‘Luteni Kalama’, wiki iliyopita ndani ya Ukumbi wa Kakala uliopo Kigamboni, Dar  lakini dakika 20 kabla ya tukio hilo alinaswa katika kona moja ya ukumbi huo akidendeka na mchepuko ambaye pia ni Mbongo Fleva, Inspector Haroun. 

Paparazi wetu ambaye alikuwepo ukumbini hapo aliwanasa wawili hao katika kona moja yenye giza  wakiwa ‘mahaba niu’e huku Inspector akionekana kuwa na wasiwasi wa kuonwa na mwenye mali. 

Baada ya kushtushwa na mwanga wa kamera, wawili hao walionekana kuweweseka kwanza kisha, Inspector akaanza kumwomba paparazi wetu kuzifuta picha hizo akidai zikionekana zinaweza kumletea matatizo.
“Kaka soo bwana… soo kaka! Huyu ni shemeji yangu, hapa tuna hang’ tu… noma mkubwa.  Hizo picha zikionwa nitafikiriwa vibaya na ‘mwanangu’ (Kalama),” alisema Inspector kwa sauti ya unyenyekevu. Bella yeye alisema: “Halafu hawa kwa kufuatafuata watu hawajambo. Futa bwana hizo picha.”

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.