Tuesday, April 14, 2015

Anonymous

TUHUMA ZA KUIBA MUME WA MTU: MSANII MWENYE MVUTO, TONTO DIKEH AWANANGA MAADUI ZAKE!

Mwigizaji maarufu wa filamu nchini Nigeria Tonto Dikeh.
TONTO DIKEH, mwigizaji maarufu wa filamu nchini Nigeria, ambaye ni ‘mcharuko’ na ambaye alidaiwa kumchukua mume wa mtu hivi karibuni, hivi sasa amekuwa kama mhamasishaji ambapo anatoa ujumbe mbalimbali wa kuwatia matumaini mashabiki wake kupitia ukurasa wake wa Instagram.
Tonto ambaye ni mzaliwa wa Jimbo la River na aliyepata umaarufu zaidi kwa kuigiza filamu ya ‘Dirty Secrets’, amewaasa mashabiki wake kutojali mambo mabaya wanayosemwa na watu na kwamba “wanachokifikiria watu kuhusu wewe si shauri lako.” 

Alisisitiza kwamba,  “Kuna watu fulani ambao duniani hawana la kufanya zaidi ya kutukana wenzao.  Iwapo watakusema vibaya jua hawana uwezo wa kufanya mambo ya maana unayoyafanya.  Watu hao watakuchekea usoni, lakini moyoni wanakuogopa.” 

Ameongeza: “Watu wasioweza chochote, huyaona mabaya tu miongoni mwa mema unayofanya, wakisema wanavyoweza kuyafanya unayofanya iwapo wakitaka.  Ukweli hawawezi kuyafanya hayo, kwani wangekuwa na uwezo wa kuyafanya, wangeyafanya bila ya kupiga kelele. “Wanachoweza kufanya ni kuzungumza tu.  Cha kufanya ni kuzidi kung’arisha jina lako kwani watu hao ni dhahiri wanakuzimia; kwa sababu  wivu na hiyana vinawamaliza.”

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.