Ney wa Mitego mbele ya nyumba yake
Matanuzi ni sehemu ya maisha ya mastaa wengi duniani, hivyo hata
wanapoamua kufanya mambo ya maendeleo, hukakikisha wanafanya yale
yatakayoendana na hadhi zao. Wapo wanaoamua kutanua kwa akili kwa
kuwekeza katika vitu vya msingi kama nyumba na vitega uchumi.Tofauti na miaka iliyopita, mastaa wa Bongo, sasa hujiona wamefanikiwa ikiwa watamiliki ardhi au nyumba za kifahari tofauti na miaka ya nyuma.
Leo hii hata wanaomiliki magari makali, ukiwachunguza kwa undani utagundua tayari wameshawekeza katika ardhi na wameshaanza ujenzi wa nyumba za kifahari.
Starehe inakuletea orodha mastaa 10 wa Bongo wanaomiliki nyumba za kisasa, zenye thamani kubwa. Orodha hii haina haijazingatia nafasi zao.
Lady Jaydee
Ni msanii anayejiheshimu na aliyejijengea imani kubwa kwa mashabiki wake na wapenzi wa muziki Afrika. Fedha yake ya awali kabisa aliyoichuma kupitia muziki, aliwekeza kwenye ardhi na kuwa msanii wa kwanza Bongo aliyemiliki nyumba ghali maeneo ya Kimara jijini Dar es Salaam. Hata hivyo, hakuwahi kutangaza thamani ya nyumba hiyo. Pia anatajwa kumiliki mali kadhaa.
Profesa Jay
Aliwahi kutangaza kwamba nyumba yake aliyoijenga Mbezi ya Kimara jijini Dar es Salaam ina thamani ya Sh100 milioni. Huyu alikuwa miongoni mwa wasanii wa mwanzo kabisa kutangaza kumiliki nyumba zao wenyewe, hali iliyoongeza mwamko kwa wasanii wengine wachanga kuwekeza katika ardhi.
Madee
Ni mwanamuziki mkongwe kutokea katika kundi la Tiptop Connection. Pia anajulikana zaidi kwa jina la Rais wa Manzese, anamiliki nyumba ya kisasa iliyopo maeneo ya Mbezi, Dar es Salaam. Ni nyumba ambayo hajawahi kutaja kiasi cha fedha halisi kilichotumika kuikamilisha licha ya kuonekana kuwa imegharimu fedha nyingi.
Diamond
Mwaka 2015 umekuwa ni mwaka wa staa huyu baada ya kufanikiwa kuhamia katika nyumba yake iliyopo katika eneo la wa Madale Tegeta, Dar es Salaam. Nyumba hiyo ambayo imedaiwa kuwa na choo kilichonakshiwa kwa dhahabu yenye thamani ya Sh 70 milioni.
Kwa mujibu wa msanii huyo, nyumba hiyo imegharimu zaidi ya Sh280 milioni, imechukua takribani miaka miwili kumalizika na ina bwawa la kuogelea, Gym, Dancing Hall, Studio, DartsCourt na BasketBall Court.
Nay wa Mitego
Ni mwanamuziki wa hiphop ambaye amefanikiwa
kuwajuza mashabiki kwamba aina hiyo ya muziki kwa sasa inalipa baada ya
kujenga nyumba ya kifahari iliyogharimu kiasi cha Sh180 milioni. Kwa
mujibu wa Ney wa Mitego, alianza kujenga nyumba hii tangu mwaka 2013 na
ni miongoni mwa nyumba zake tatu, huku nyumba zake mbili zikiwa bado
hazijakamilika.
Masanja Mkandamizaji
Masanja Mkandamizaji
Licha ya kumiliki mashamba makubwa ya mpunga na
miradi kadhaa, Masanja Mkandamizaji anamiliki nyumba tatu za maana Dar
es Salaam, moja ni ghorofa iliyopo maeneo ya Tabata, nyingine Kigamboni
na nyingine haifahamiki eneo ilipo.
Hata hivyo, imebainika kuwa mbali na mijengo yake hiyo , nyumbani kwao Mbarali, Mbeya ana mjengo wa maana.
Juma Jux
Juma Jux
Mwanamuziki Juma Jux yeye ni mmoja kati ya wasanii
waliofanikiwa kupitia kazi zao za sanaa, baada ya kujenga jumba la
kifahari lenye ghorofa moja ambalo mpaka sasa bado haijajulikana liko
eneo gani jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa Jux, jumba hilo litakuwa
na studio, bwawa la kuogelea, gym na sehemu zingine muziki kama
alivyotangaza.
Chege na Temba
Chege na Temba
Hawa ni wasanii wanaotokea katika kundi la TMK
Wanaume Family lililo chini ya Said Fella. Wawili hawa wanamiliki nyumba
mbili kila mmoja. Fella anasema amekuwa akifanya hivyo kwa wasanii
wengine ambao walishatoka ndani ya kundi hilo wapatao saba.
“Nilishawakabidhi waliotoka sitaki kuwataja kila siku maana wananambiaga kwanini nawataja, lakini nishafanya hivi kwa wasanii wangu siyo chini ya saba. Thamani yake bado hatujakaa kupiga mahesabu maana ujenzi wake ni wa kimaskini na ufahamu tukipata Sh102,000; Sh20,000 tunanunua matofali na Sh80,000 tunakula na watoto. Ina vyumba vitatu vya kulala, sehemu ya chakula, parking ya magari. Temba na Chegge wana nyumba mbili mbili,” anasema Fella
“Nilishawakabidhi waliotoka sitaki kuwataja kila siku maana wananambiaga kwanini nawataja, lakini nishafanya hivi kwa wasanii wangu siyo chini ya saba. Thamani yake bado hatujakaa kupiga mahesabu maana ujenzi wake ni wa kimaskini na ufahamu tukipata Sh102,000; Sh20,000 tunanunua matofali na Sh80,000 tunakula na watoto. Ina vyumba vitatu vya kulala, sehemu ya chakula, parking ya magari. Temba na Chegge wana nyumba mbili mbili,” anasema Fella
Idris Sultan
Mshindi wa Big Brother Hotshots aliyefanikiwa kujipatia kitita
cha dola za Marekani 300,000 hivi sasa anamiliki jumba lenya ghorofa
moja. Hata hivyo, nyumba hiyo bado hajazungumzia kuhusu gharama halisi
alizotumia kuinunua.
AY
AY
Huyu ni kati ya wasanii wanaomiliki fedha, kampuni
na mali kibao lakini hawapendi kujionyesha imefahamika. Chanzo makini
na cha karibu na msanii huyo kimesema kuwa AY ni msanii anayemiliki
biashara nyingi ndani na nje ya nchi.
Anadaiwa kumiliki nyumba na viwanja kadhaa hapa jijini sambamba na maduka kadhaa Nairobi Kenya.
Anadaiwa kumiliki nyumba na viwanja kadhaa hapa jijini sambamba na maduka kadhaa Nairobi Kenya.
AY aliwahi kukaririwa akisema kuwa ana mpango wa
kununua nyumba Kenya na kufungua maduka kwa kuwa ni sehemu ambayo
anakwenda sana kwa ajili ya shughuli zake mbalimbali.


Note: Only a member of this blog may post a comment.