Sunday, April 19, 2015

Anonymous

MSANII PREZZO AZIDI KUONYESHA NIA YAKE YA KUINGIA KWENYE SIASA


CMB Prezzo.
MAPEMA mwaka jana, rapa wa nchini Kenya, CMB Prezzo katika mahojiano yake redioni alisema atakuwa akiwania nafasi ya kisiasa katika uchaguzi mkuu ujao.
Mbali na kuwa alisema siku moja atawania nafasi ya urais, baadhi ya vyanzo vya habari vimeeleza kuwa kwa sasa staa huyo anajiandaa kuzindua kampeni yake ya kuingia kwenye siasa.
Prezzo mwenyewe amethibitisha taarifa hizo kwa kusema: "Ni kweli nina mpango wa kuingia kwenye siasa"
"Kwa sasa bado nashauriana na washauri wangu wa kisiasa na nikiwa tayari na kujua ni nafasi gani niwanie, nitaujulisha umma", alisema mwanamuziki huyo.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.