Polisi wa kizungu wa South Carolina nchini Marekani, jana Jumanne
alishtakiwa kwa kosa la mauaji, saa chache baada ya maofisa kutazama
video ya kushangaza inayomuonesha akimpiga risasi mgongoni na kumuua
mwanaume mwenye asili ya Afrika aliyekuwa akikimbia.
Meya wa North Charleston, Keith Summey alitangaza mashtaka hayo kwenye mkutano na waandishi wa habari ambapo alisema polisi huyo aitwaye Michael Thomas Slager alichukua uamuzi mbaya. Aliyeuawa anaitwa Walter Lamer Scott mwenye umri wa miaka 50.
Video hiyo iliyosambazwa kwenye vituo vya runinga inamuonesha ofisa hiyo akimmiminia risasi mgongoni mtu huyo wakati akikimbia.
Mtu aliyechukua video hiyo hajulikani.
Meya wa North Charleston, Keith Summey alitangaza mashtaka hayo kwenye mkutano na waandishi wa habari ambapo alisema polisi huyo aitwaye Michael Thomas Slager alichukua uamuzi mbaya. Aliyeuawa anaitwa Walter Lamer Scott mwenye umri wa miaka 50.
Video hiyo iliyosambazwa kwenye vituo vya runinga inamuonesha ofisa hiyo akimmiminia risasi mgongoni mtu huyo wakati akikimbia.
Mtu aliyechukua video hiyo hajulikani.


Note: Only a member of this blog may post a comment.