Mwandishi Wetu
Pole sana mama! Staa wa sinema za Kibongo, Wema Isaac Sepetu
‘Madam’ amefunguka kuwa mama yake mzazi, Miriam Sepetu anasumbuliwa na
macho ambapo madaktari wamegundua kwamba amepoteza uwezo wa kuona kwa
asilimia sabini na tano (75%).“Kumnusuru mama yangu asipate upofu wa moja kwa moja inabidi afanyiwe operesheni ya macho,” alisema Wema kwa huzuni kwa kuwa hakuna kama mama.

Note: Only a member of this blog may post a comment.