Monday, April 27, 2015

Anonymous

MAMBO HADHARANI: MZEE MAJUTO AFUNGUKA KUOA MJUKUU WAKE!

Mayasa Mariwata
Vunja ukimya! Komediani namba moja Bongo, Amri Athuman ‘Mzee Majuto’ amegeuka mbogo baada kuulizwa juu ya madai ya kuoa binti mdogo ambaye ni sawa na mjukuu wake mwenye umri wa miaka 18 akidai kuwa sheria ya dini inamruhusu kufunga ndoa wa wake wanne.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda ambalo ndilo lililokuwa la kwanza kuripoti ishu hiyo, Mzee Majuto ambaye awali alionesha kuwa na jazba alifunguka:
“Hilo suala haliwahusu wala na si jambo la ajabu kabisa kwa sababu mimi ni mwanaume wa Kiislamu, sheria ya dini inaniruhusu kuoa mke wa kwanza wa pili wa tatu hadi wanne,” alisema Majuto

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.