Wakati mchakato wa CCM kutafuta mgombea
Urais ukitarajiwa kuanza mwezi ujao, imebainika kuwa kuna mkakati wa
kuyapiga chini makundi ya makada wanaosaka urais ili kupata mgombea
ayakayekinusuru chama hicho katika uchaguzi mkuu Oktoba mwaka huu.
CCM imekuwa ikipata wakati mgumu kila
mwanachama wake anapomaliza vipindi vyake viwili vya urais, na safari hii
kazi ya kumpata mrithi wa Rais Jakaya Kikwete ambaye
amepata urais mwaka 2005 inaonekana kuwa ngumu zaidi na huenda
ikasababisha chama hicho kupunguzwa nguvu zaidi iwapo haitafanya uamuzi
unaokubalika na makundi yote ya Urais.
Makundi makubwa yanayolengwa na mkakati
huo wa kuyapiga panga, ni ya makada wanaoonekana kuwa na nguvu na
ushawishi mkubwa ambayo kambi zao zimekuwa zikipambana vikali kwenye
vita ya chini kwa chini ya Urais.
Makundi hayo ni lile linalomuunga mkono Lowassa na linalomuunga mkono Membe,watu
wanauwaunga mkono makada hao wamekuwa wakipishana mikoani kuweka mambo
sawa kwa vigogo hao, hali ambayo inaonekana kuwatisha CCM kiasi cha
kuchelewa kutangaza kwa mchakato wa Urais ndani ya chama hicho.
Tayari makada hao na wenzao wamepwa onyo
kali inayowazuia kuwania nafasi yoyote kwa kipindi cha miezi 12 na
adhabu hiyo ilikuwa imalizike Februari mwaka mwaka huu lakini imeongezwa
muda kutokana na kamati ya maadili kuendelea na uchunguzi.
-MWANANCHI



Note: Only a member of this blog may post a comment.