Monday, April 13, 2015

Anonymous

INATISHA SANA! POLISI WANYANG’ANYWA WATUHUMIWA, WACHOMWA MOTO HADI KUFA KILIMANJARO! #NewUpdates

Hii ni updates kama tulivyowaahidi tulivyotoa taarifa ya awali kuhusu ishu hii...Tuendeleee...
Makongoro Oging
Hii  si poa! Raia wenye hasira, katikati ya wiki iliyopita waliwachukua vijana wawili wanaotuhumiwa kuwa majambazi, waliokuwa mikononi mwa polisi, ambao majina yao yametajwa kuwa ni Mnubi na White kisha kuwateketeza kwa moto baada ya kuwabaini kuwa ndiyo waliohusika na uvamizi na uporaji wa maduka mawili ya huko Mwika-Madukani, Moshi vijijini.


Chanzo chetu kililiambia gazeti hili kuwa, vijana hao wakiwa na silaha, walionekana wamepanda pikipiki moja na kuvamia maduka hayo mawili na kupora fedha kiasi ambacho bado hakijajulikana, kabla ya kutoweka.

Kesho yake walikamatwa na wananchi walioshirikiana na polisi, baadaye kukatokea kutoelewana baada ya jeshi hilo kutaka kuwachukua ili kuwapeleka mbele ya sheria.


“Polisi waliwaweka katika gari lao ili waondoke nao, lakini wananchi waliwachomoa na kuwapa kipigo kisha kuwateketeza kwa moto, askari walijaribu hata mabomu ya kutoa machozi, lakini wakazidiwa,” kilisema chanzo hicho.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Godfrey Kamweli alikiri kutokea kwa tukio hilo.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.